kwangila

Just another WordPress.com weblog

NAMNA YA KUPIMA UBORA WA MAISHA.

Kunavyo vigezo mbambali wanavyotumia watu kupima ubora wa maishayao. Baadhi yetu tutatumia mali tuliyonayo kama vile majumba, biashara na mafedha tuliyoweka benki. Wengine tutapima maisha kwa vyeo tulivyo navyo katika jamii kwa mfano mwanasiasa atajiona kuwa bora zaidi kuliko raia wa kawaida. Kisha kunao watatumia elimu kudai kwamba maisha yao ni bora. Hivyo basi profesa atajiona kuwa miongoni mwa watu wachache walio na maisha bora . Wengine watatumia vigezo vya familia. Hivyo basi dume lililo na mke mrembo au watoto watiifu na werevu shuleni atajiona kuwa bora zaidi. Lakini swali linabakia kuwa kilele cha maisha bora ni nini? Ni mapesa, ni vyeo, ni familia, elimu?

         Kwa mujibu wa wanasaikolojia, ubora wa maisha ni jumla ya vipengele vingi. Kipengele kimoja ni jiwe lisiloweza kuijika chungu. Hii ndiyo sababu tajiri aso mke hatakuwa na maisha bora. Hii ndiyo sababu Profesa asokuwa na mali hatajihesabu kuwa na maisha bora. Mwanasiasa asiyekuwa na elimu atajiona duni katika bunge na mara nyingi atanyamaza kimya mijadala inapoendelea bungeni.

         Ukitaka kujua watu uliodhani wana maisha bora sivyo ilivyo, nenda nchini Kenya umpate bwana wa umri wa zaidi ya miaka 50 aliyeamua kujiunga na shule ya msingi licha kwamba anamali. Njoo Marekani ukutane na wanawake wenye dola lakini wameishia katika vyumba vya washauri maanake hawana wenzi katika maisha yao. Rudi nchini Kenya tena ukutane na rais Kibaki ambaye licha ya kudhani kwamba maisha bora ni kuwa rais, ametajwa na upinzani kuwa mhusika katika ufisadi serikalini. Kisha baada ya safari hizo tatu ujilize kwa nini wasomi wengi siku hizi wanajitia kitanzi? Wengi wanajitosa majini, wengine wanajitia mikanda shingoni huku wengine wakibugia sumu.  

            Kwangu mie nikidhani wa ubora maisha hupimwa kwa kiwango cha furaha alicho nacho mtu. Si lazima uwe na mali nyingi kupindukia wala elimu ya hali ya juu ili uwe na furaha. Vilevile furaha hailetwi na cheo alicho nacho mtu katika jamii wala kuwa na familia pekee.

April 15, 2006 Posted by Daudi Kyeu | Uncategorized | | 2 Comments