kwangila

Just another WordPress.com weblog

KIFO NI NINI?

Ni peremende tunayoibeba mikobani kila sekunde. Hakibagui tajiri wala maskini. Hakibishi hodi wala hakiambiwi subiri kidogo. Hakitumii aina moja ya usafiri kinapoabiri. Kinawaanua walio kwenye orofa kwa mitetemeko ya ardhi. Kinawazuru maskini kwa kutumia ukame. Kinawatumbuiza mabwanyenye kupitia magonjwa. Kinawamaliza wabunge kwa ajali za ndege. Kinamaliza mataifa makubwa kwa milipuko ya mabomu. Kina nguvu za kuvunja milango ya vyuma tuliyojiwekea. Kinawakamata marais licha yao kuzingirwa na walinzi. Kina mdomo wazi wa kuimeza meli nzima baharini. Umri kwacho si hoja. Kinamtonoa kijana na kumwacha mzee. Hakina huruma eti. Kinafagia familia na kuyaacha mabilioni ya pesa benki.

Kifo ni siri ya MUNGU. Kina vyombo anuwai vya kuabiria. Kikizuru kwangu siku imefika ndugu. Hamna nafasi ya kukiambia njoo mtondogoo.

April 12, 2006 Posted by Daudi Kyeu | Uncategorized | | 17 Comments