MIAKA 14: UMRI WA MTOTO KUFANYA KAZI MAREKANI.
Iwapo serikali za bara Afrika zina lengo la kupunguza umaskini, ipo haja ya kuhakiki baadhi ya sheria ambazo hazina mantiki kamwe. Nchini Kenya kwa mfano, raia wamelazimishwa kuamini kwamba ni kinyume cha sheria kumwajiri mtoto akiwa na umri wa chini ya miaka 18. Kwa king'eng'e wanaiita hali hii 'child labor'.
Kutowatambulisha watoto katika ulimwengu wa kazi kumewafanya kuwa wazembe kiasi cha kununuliwa chupi na mama zao. Nina maana ya watoto walio kati ya umri wa miaka 14-18. Hali hii imepelekea wazazi kutumia rasilimali nyingi kwa watoto kiasi cha kusahau kujali maslahi yao pia. Chukulia kwa mfano mzazi aliye na watoto wanne walio kati ya miaka 14 na 18. Kisha mzazi huyu mshahara wake ni dola 100 kwa mwezi. Mzazi hataweza kuwakidhia watoto hawa mahitaji kwa ubora unaohitajika.Watoto hawa wana umri tosha wa kwenda kusaka kazi hata kama ni ya uyaya au kuosha vyoo. Mradi wapate fedha za kukidhia mahitaji yao.
Nchini Marekani umri wa mtoto kufanya kazi ni miaka 14. Wengi wa watoto walio na umri huu ni wa shule za upili. Baada ya shule jioni, watoto hawa hujitoma katika soko la kazi kutafuta dola. Utawapata wakiosha vyombo katika hoteli, wakifanya uyaya wa muda au kuwatembeza mbwa wa jamaa fulani. Wao hufanya kazi kwa muda kabla ya kwenda nyumbani kufanya mazoezi waliyopewa shuleni. Tajriba hii anayopata mtoto wa Kimarekani humwongezea sifa katika kapu lake siku za usoni atakapotazamia kutafuta kazi ya kudumu.
Nchini Kenya, vitoto vingi hata vyenye umri wa zaidi ya miaka 20 hutarajia wazazi wao kuwakidhia kila takwa. Wanaponing'onozewa kwamba hoteli fulani inahitaji mfanyikazi wa muda vitoto hivi huona hii ni kazi ya wasio na elimu. Itakuwa heri kwao kucheza basketi boli, au kutazama runinga kisha jioni wende nyumbani kuandaliwa chakula.
No comments yet.
Leave a comment
-
Recent
- MAREKANI INAVYOFADHILI VITA BARANI AFRIKA.
- MISHAHARA YA WABUNGE KENYA: WIZI! WIZI! WIZI!
- SIKUKUU YA KUVUTA MARIJUANA MAREKANI.
- UBAKAJI: NJOKI NDUNG’U ANAFICHA HABARI FULANI.
- MADHARA YA KUWEPO SARAFU AINA MOJA AFRIKA MASHARIKI.
- KUNA HATARI YA KALONZO MUSYOKA KUWA RAIS?
- NAMNA YA KUPIMA UBORA WA MAISHA.
- KIFO NI NINI?
- KITOTO CHA MAREKANI KINASAFIRI ULIMWENGUNI ZAIDI YA MHADHIRI CHUONI AFRIKA.
- KUTOJUMULISHA MIKOPO YA WAFADHILI: HEKO SERIKALI
- MBONA MAREKANI NA UINGEREZA ZINAINGIA TANZANIA BILA BREKI?
- KAMUSI YA ISIBATI
-
Links
-
Archives
- May 2006 (2)
- April 2006 (14)
- March 2006 (12)
-
Categories
-
RSS
Entries RSS
Comments RSS