SEHEMU ZA SIRI ZANYIMWA HAKI MAREKANI.
Haya ndiyo maendeleo wanayojivunia. Ya wanaume kuwa na uhusuano wa kimapenzi na wanaume wenzao. Yashangaza kuwaona wanawake wakikiuka kanuni za kimapenzi; kwamba sharti mwanamke aridhishwe kiu na mwanamume bali sio mwanamke mwenzake. Hii ndiyo demokrasia wanayoizungumzia na kuitangaza kote ulimwenguni. Dhambi ya aina hii imeambukizwa vijana pia huku Marekani na huwezi katu kuwakaripia maanake sheria za nchi zinalinda demokrasia,
kama wanavyosema. Unapotazama filamu zao mojawepo ya maudhui ni ngono za jinsia moja.
Inapotukia ngono kati ya mwanamume na mwanamke, mambo yanakuwa ya firauni sasa. Midomo imechukua nafasi ya sehemu za siri ya mwanamke na mwanamume.Yashangaza kusikia jinsi hawa 'walioendelea' ni wachafu hasa katika midomo
yao. Mbona mwanamke anyonye shakawa za mwanamume huku mwanamume akipata uhondo katiba kukiramba kile kidude. Ikizidi wataziramba ngoko pia; kunakotokea kinyesi. Nimekuwa makini sana kutompa busu yeyote hapa Marekani maanake sijui dakika chache zilzopita alikuwa akifanya kazi gani na siko tayari kupakwa kinyesi katika shavu langu mie.
Kuna msamiati huku kwa jina sherehe za kimapenzi au kwa king'eng'e wanaziita 'sex parties'. Hapa swala kuu si kuonja vyakula mbalimbali vilivyotayarishwa bali ni kumuonja yeyote yule aliyekuja. Hamna faragha hapa. Ngono zitafanywa wazi sakafuni, kutani, vitandani kwenye makochi n.k. Juzi kumekuwa sherehe hapa chuoni Brown. Waliita sherehe
yao 'Gay Students Association'. Ili uweze kukubalika, ulihitajika kuja pale ukiwa uchi au chupi na kanchiri pekee. Nilikuwa pale kushuhudia jinsi 'demokrasia' imekengeusha wanafunzi Wamarekani.
Usimwone binti na ghulamu wamekubatiana ukadhani itakuwa hivi hadi kifo kitakapowatenganisha. Jana binti huyu alikuwa na boifrendi tofauti na juzi na atakuwa tofauti pia ijapo kesho kutwa. Katika ndoa ni vivyo hivyo. Iwapo mwanamume ameanza kulegea basi huenda akaletewa ndume kazi kitandani mwake. Katika matangazo yao utaona tangazo
kama hili;
"Mimi na mume wangu tumeamua kuwa na mhusika wa tatu katika ngono. Ningependa
kumtazama mume wangu akifanya ngono na mwanamke mwingine…."
Mniambie Wakristo nikidhani pia Waislamu, je haya yanakubalika katika dini? Licha kwamba wenzetu hawa ni matajiri wa tekinolojia wao ni maskini hohehahe wa kimaadili. Nina uhakika bara la Afrika ndilo linaongoza ulimwenguNI katika kuwa na utajiri mkubwa wa maadili ya jamii.
9 Comments »
Leave a Reply
-
Recent
- MAREKANI INAVYOFADHILI VITA BARANI AFRIKA.
- MISHAHARA YA WABUNGE KENYA: WIZI! WIZI! WIZI!
- SIKUKUU YA KUVUTA MARIJUANA MAREKANI.
- UBAKAJI: NJOKI NDUNG’U ANAFICHA HABARI FULANI.
- MADHARA YA KUWEPO SARAFU AINA MOJA AFRIKA MASHARIKI.
- KUNA HATARI YA KALONZO MUSYOKA KUWA RAIS?
- NAMNA YA KUPIMA UBORA WA MAISHA.
- KIFO NI NINI?
- KITOTO CHA MAREKANI KINASAFIRI ULIMWENGUNI ZAIDI YA MHADHIRI CHUONI AFRIKA.
- KUTOJUMULISHA MIKOPO YA WAFADHILI: HEKO SERIKALI
- MBONA MAREKANI NA UINGEREZA ZINAINGIA TANZANIA BILA BREKI?
- KAMUSI YA ISIBATI
-
Links
-
Archives
- May 2006 (2)
- April 2006 (14)
- March 2006 (12)
-
Categories
-
RSS
Entries RSS
Comments RSS
Karibu David. Tumekusubiri sana kumbe ulikuwa unablogu kichinichini. Haya karibu kiwanjani na ujisikie kuwa uko nyumbani. Hata kama nyumbani ni kichakani, Nyumbani ni nyumbani. Blogu yangu ilibadili jina na sasa yapatikana hapa: http://mwaipopo.blogspot.com/
Kwangila/David/Mtandawazi, karibu sana kwenye kijiji cha blogu na kwenye wordpress. Karibu hadi ndani, wala viatu usitoe.
umeingia kwa kasi sana kaka , karibu ukumbini , wacha nikimbie kuorodhesha na kutangaza blogu hii huko kwingine .
[...] kwenye posti yake Sehemu za Siri zanyimwa Haki Umarekani ameandika kuhusu vile maadili yanavyozidi kuzikwa huko ughaibuni , wiki iliyopita nilibaki kushangaa tu baada ya kusoma posti kadhaa za wakenya wenzetu ambao wameamua kuiga tabia hizi na kujaribu kujitetea kiholela eti ni haki yao ya kidemokrasia , jambo hili lilikuwa kwenye orodha ya vile vitu vingi ambavyo nimepanga kuviandikia siku za mbeleni itakuwaje tuige bila kufikiria tabia zao , elimu yao ndio ni zuri kushinda yetu majumba yao yananguvu kushinda yetu lakini maadili yao maovu si lazima tuyaige kwani tukiyafuata tutakuwa tumekosa mbele wa nyuma tytakuwa kama kondoo waliopoteza mchungaji . nafkiri sentensi yake ya mwisho ndio imebeba ukweli mwingi kwani anamalizia kwa kusema Licha kwamba wenzetu hawa ni matajiri wa tekinolojia wao ni maskini hohehahe wa kimaadili. Nina uhakika bara la Afrika ndilo linaongoza ulimwenguni katika kuwa na utajiri mkubwa wa maadili ya jamii. [...]
Pingback by mawazo na mawaidha » blogu mpya | March 27, 2006 |
Mtandawazi, jamvi tushalinyoosha, mapochopocho tukatayarisha na sebule tukaiandaa vyema…karibu ni usijisikie mgeni sana kwani wote ni wakarimu katika ukumbi wa blogu//
Mila na desturi za kigeni zisipochujwa kwa makini husababisha majanga makuu sawa na yale ya Kipini au watu wanabii Luti. Mbona mwelekeo tukaupoteza?
[...] Maitha, points to a possible increase in the number of Kenyan bloggers blogging in Kiswahili, a major language in East Africa. He welcomes the newest entrant Mtandawakazi Maitha shares his thoughts on the discussion that has been going on about sexuality and its place in Africa. The 2 posts he points to that contain these discussions are “Outing hetero-sexuality” by Mad Kenyan Woman, and “homo-sexuality is un-african“, by Gukira a very rough translation being “We should not follow western behaviour, their education is better than ours, but we should not emulate this behaviour, if we just follow, we will have lost direction, like sheep without a shepherd”. [...]
Pingback by Open Blog: KenyaUnlimited » Kenyan Blogosphere Dispatch | March 28, 2006 |
[...] Maitha, points to a possible increase in the number of Kenyan bloggers blogging in Kiswahili, a major language in East Africa. He welcomes the newest entrant Mtandawakazi Maitha shares his thoughts on the discussion that has been going on about sexuality and its place in Africa. The 2 posts he points to that contain these discussions are “Outing hetero-sexuality” by Mad Kenyan Woman, and “homo-sexuality is un-african“, by Gukira a very rough translation being “We should not follow western behaviour, their education is better than ours, but we should not emulate this behaviour, if we just follow, we will have lost direction, like sheep without a shepherd”. [...]
Pingback by Global Voices Online » Blog Archive » Kenyan Sphere Dispatch | March 28, 2006 |
Perfect pages… tnx
Get more information about ethiopia on this blog