ELIMU SIO MUHIMU NCHINI KENYA
Nchini
Kenya elimu si muhimu hata kidogo. Licha ya serikali kutumia fedha nyingi kuwaelimisha wanafunzi, wanafunzi hawa hawapewi nafasi ya kulijenga taifa kulingana na elimu waliyoipata. Hata uwe Professa mwenye digrii milioni moja hamna wa kutambua maarifa uliyo nayo angaa akupe nafasi ulikwamue taifa hili kutokana na tope la umaskini. Mfano ni Wangari Maathai ambaye juzi amepewa tuzo la kimataifa. Ole wake maanake Serikali ya Kibaki haitambui umaarufu wake na anachoweza kupata sasa ni unaibu wa waziri mbali si Uwaziri.
Kuna binti hivi majuzi aliteuliwa kuwa mnaibu wa wizara ya vijana kisha akahamishwa mara moja hadi wizara isiyolingana na elimu yake. Nina uhakika Mbarire angetekeleza majukumu vizuri iwapo angeachwa pale maanake kipawa na elimu yake i pale.
Yashangaza kusikia sekretari aliye na cheti pekee ndiye Waziri wa afya ilahali kuna wabunge jamani waliosomea Utabibu. Maina Kamanda ni naibu wa waziri pia licha kwamba elimu yake imepigiwa maswali. Kalembe ndile ni waziri wa utalii licha kwamba hana uwezo wa kuhamasisha ulimwengu kuhusu uhifadhi wa mazingira. Hata ingawa Prof Kivutha Kibwana ameisomea Sheria na uundaji wa katiba alichoweza kupata katika serikali hii ni uhifadhi wa miti.
Tumearifiwa katika gazeti la Standard kwamba uteuzi wa Mabalozi unategemea unasaba wako na watu maarufu katika serikali. Aliteuliwa kakake Wilfred Machage, Kisha Mwakwere akamteua dadake, balozi mjini
Tokyo ni wa familia ya Moody Awori n.k. Uteuzi wa makatibu wa wizara vilevile si katika misingi ya elimu bali ni jinsi ulivyojiweka katika mtandao. Simeon Nyachae aliwaleta Wakisii kadhaa ambao wana unasaba, naye Musikari Kombo alikuwa ameapa kutokubali Uwaziri iwapo Waluhya hawatapewa nafasi kadha kama wakurugenzi wa mashirika ya serikali.
Kiraitu Murungi alipokuwa Waziri wa Sheria amewaleta Wameru kibao katika wizara hii, swala ambalo huenda likampa kazi maradufu Waziri mpya Martha Karua.
Haikosi hii ndiyo sababu wasomi wengi wasio katika mtandao wametorokea nchi za kigeni kutafuta ajira. Kumbuka wengi wa wasomi hawa walielimishwa kwa mikopo ya serikali na badala ya kupewa nafasi ya kufaidi umma kwa elimu waliyoipata serikali inawaajiri ndugu za mawaziri. Walio na elimu nchini Kenya ndio wanalisukuma taifa kwa kodi wanayotozwa licha ya mishahara
yao kuwa midogo. Mifano ya watu hawa ni walimu. Wasomi tuamkeni tudai haki yetu. Haiwezekani taifa kusonga mbele iwapo halitumii elimu ya raia wake na kuilipia elimu ile ipasavyo.
1 Comment »
Leave a comment
-
Recent
- MAREKANI INAVYOFADHILI VITA BARANI AFRIKA.
- MISHAHARA YA WABUNGE KENYA: WIZI! WIZI! WIZI!
- SIKUKUU YA KUVUTA MARIJUANA MAREKANI.
- UBAKAJI: NJOKI NDUNG’U ANAFICHA HABARI FULANI.
- MADHARA YA KUWEPO SARAFU AINA MOJA AFRIKA MASHARIKI.
- KUNA HATARI YA KALONZO MUSYOKA KUWA RAIS?
- NAMNA YA KUPIMA UBORA WA MAISHA.
- KIFO NI NINI?
- KITOTO CHA MAREKANI KINASAFIRI ULIMWENGUNI ZAIDI YA MHADHIRI CHUONI AFRIKA.
- KUTOJUMULISHA MIKOPO YA WAFADHILI: HEKO SERIKALI
- MBONA MAREKANI NA UINGEREZA ZINAINGIA TANZANIA BILA BREKI?
- KAMUSI YA ISIBATI
-
Links
-
Archives
- May 2006 (2)
- April 2006 (14)
- March 2006 (12)
-
Categories
-
RSS
Entries RSS
Comments RSS
Si kubaliani nawe kabisa ……Unamaanisha kwamba ikiwa kakako ni waziri basi ni hatia kuteuliwa kufanya kazi yoyote….?