BIASHARA YA ELIMU: TUIGE MAREKANI
Ukweli ni kwamba popote walipo Marekani sharti wawe na lengo la kupata faida. Iwapo sivyo, watafunganya virago na kuondoka. Nchi hii imejiendeleza katika kila hali kwa kuwekeza mtaji katika biashara za kilimwengu. Kila taasisi Marekani imeajiri wataalam wa biashara kwa lengo la kupata maarifa ya jinsi ya kufanya biashara.
Baadhi ya biashara ambazo Marekani wamefanikiwa ni biashara ya uhamiaji, biashara ya shule za kimataifa katika nchi geni, biashara ya mitihani k.v. TOEFL, SAT, GRE , biashara ya kutoa mikopo kwa mataifa maskini n.k. Vyuo vikuu vimechangia pakubwa pia katika kuujenga uchumi wa Marekani.
Katika makala hii nitafafanua jinsi vyuo vikuu vinafanikisha biashara za Wamarekani. Vyuo hivi hutangaza nafasi kwa walimwengu bali sio kwa Wamarekani pekee. Wamefanikiwa kufanya hivi kwa kuweka vyuo hivi vyote katika mtandao kiasi kwamba mwenye kiu ya elimu atapata habari kuvihusu kwa urahisi. Iwapo wewe si Mmarekani utahitajika kufanya mitihani kadha ili uweze kukubalika. Mtihani maarufu ni ni TOEFL ambao haujali iwapo kama ulifunzwa Kiingereza na malkia
Elizabeth mwenyewe. Mitihani hii inaizalishia Marekani mabiliono ya pesa kutoka kote ulimwenguni.
Ukishapasi TOEFL, mambo bado; utahitajika kulipa fedha za usajili chuoni zisizorudishwa. Vyuo vingi vitatoza kati ya Dola 50 na 100. Nitawapa mfano wa chuo kikuu cha Brown. Waliotuma maombi ya usajili mwaka huu walikuwa takribani 17,000. Hawa wametoka sehemu mbalimbali ulimwenguni. Hivyo basi ina maana kwamba chuo kilikusanya shilingi milioni 8,568,000 za
Kenya. Miongoni mwa hawa 17,000 ni 2,400 waliokubaliwa kujiunga na chuo. Hii ina maana kwamba 14,600 hawakubahatika licha kwamba washalipa shilingi 5,040 kila mmoja. Wengi wa hawa wasiokubaliwa ni wa kutoka nchi za kigeni.
Pesa hizi na pamoja na karo inayolipwa na waliofanikiwa, ndizo hutumika kulipa mishahara ya Wahadhiri na wafanyikazi wengine Chuoni. Kwa njia hii vyuo hivi havitegemei kamwe pesa zozote kutoka kwa serikali.
No comments yet.
Leave a comment
-
Recent
- MAREKANI INAVYOFADHILI VITA BARANI AFRIKA.
- MISHAHARA YA WABUNGE KENYA: WIZI! WIZI! WIZI!
- SIKUKUU YA KUVUTA MARIJUANA MAREKANI.
- UBAKAJI: NJOKI NDUNG’U ANAFICHA HABARI FULANI.
- MADHARA YA KUWEPO SARAFU AINA MOJA AFRIKA MASHARIKI.
- KUNA HATARI YA KALONZO MUSYOKA KUWA RAIS?
- NAMNA YA KUPIMA UBORA WA MAISHA.
- KIFO NI NINI?
- KITOTO CHA MAREKANI KINASAFIRI ULIMWENGUNI ZAIDI YA MHADHIRI CHUONI AFRIKA.
- KUTOJUMULISHA MIKOPO YA WAFADHILI: HEKO SERIKALI
- MBONA MAREKANI NA UINGEREZA ZINAINGIA TANZANIA BILA BREKI?
- KAMUSI YA ISIBATI
-
Links
-
Archives
- May 2006 (2)
- April 2006 (14)
- March 2006 (12)
-
Categories
-
RSS
Entries RSS
Comments RSS